Monday 11 May 2015

SHOGA: USIMPE NAFASI MUMEO AWE KARIBU NA NDUGUZO!

Kabla sijaanza kutiririka na mada niliyokuandalia, napenda kuwapa pole walioathirika kwa mvua iliyonyesha wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.Baada ya kutoa pole, narejea kwenye jambo ambalo nimeona ni muhimu nikaliongelea ili kuwaamsha baadhi ya shoga zetu ambao wanawapa uhuru dada au wadogo zao wa kike kuwa karibu mno na waume zao.

Ni kweli kwamba, mtu anapooa sehemu ni vyema akawa na ukaribu na ndugu wa mkewe kama kaka, wajomba, binamu, shangazi na wazazi kwani hawezi kuwakwepa kwa sababu tayari wanakuwa sehemu ya ukoo wake.

Lakini ukaribu uliopitiliza wa wanaume hao na akina dada au wadogo wa kike wa mkewe yaani mashemeji, haupaswi uzidi kipimo kwa sababu umewafanya baadhi ya shoga zetu kuangua kilio baada ya ndugu hao kujitwalia waume zao.
Shoga yangu, inakuwaje umruhusu mumeo awe anatoka out na mdogo au dada yako mara kwa mara huku wewe ukibaki nyumbani, tena wakati mwingine ndugu zako hao wakiwa wamevaa mavazi tata?

Wakitoka huko kwenye starehe wakifika nyumbani mishale mibaya wewe unawafungulia mlango ndipo dada au mdogo wako anaanza kukupa michapo ya huko kwamba; “Dada leo mume wangu kanipa ofa ya pombe na nyama choma hadi raha!”

Hivi inaingia akilini kweli, wewe unabaki nyumbani na mumeo kuondoka na nduguyo tena kwa wale waliobakirikiwa kuwa na magari nduguyo huyo huweka kishoka kwenye dirisha la mbele na miguu juu ya ‘dashibodi’ utafikiri mkewe?
Shoga, kesho na keshokutwa nduguyo akikupindua utamlaumu nani kama siyo kujilaumu mwenyewe kwa kushindwa kulinda mali zako kwani hakuna siku ambayo chui na mbuzi wanaweza kukaa pamoja bila chui kumtafuna mbuzi!
Mwenzangu, wanaume siku zote ni watu wa tamaa ambapo siyo rahisi amtoe out nduguyo ambaye si ajabu ana shepu tata kukupita wewe, akivaa kimini kinamfanya aonekane mtoto mashaallah, kumuacha hivihivi.

Kwa kifupi shoga, hilo ndilo kosa kubwa wanalofanya baadhi ya wenzetu kuwaacha ndugu zao wa kike kuwa huru kwa waume zao, wengine hawaoni kama ni hatari kumuacha mumewe na nduguye wakiangalia tamthiliya kweye tivii wakiwa peke yao sebuleni hadi usiku mnene.

Shoga yangu, usiwape nafasi ndugu zako wawe karibu kupita kiasi na mumeo, mfano kumpa huduma za nyumbani kama kumfulia nguo, kumpokea akitoka kazini, kumwandalia maji ya kuoga nk, unaweza kupinduliwa huku ukiwa bado unaipenda ndoa yako