Pamoja na kuwa kuna wanawake husita
kuolewa, lakini jambo hili si kubwa sana
kwa wanawake kama ilivyo kwa
wanaume.
Kwa kiasi kikubwa katika suala la kutaka
kuingia ndani ya ndoa, wanawake ni wengi
ambao hutaka kufunga ndoa kuliko ilivyo
kwa wanaume. Hilo tunaliona wazi tokana
wakati wa maandalizi ya shughuli za Ndoa
na Harusi.
Hata hivyo, kwa wale wanawake wachache
ambao husuasua kuolewa hizi ni baadhi ya
sababu zinazopelekea kusuasua huko.
(Izingatiwe hii ni kwa wanawake ambao
hawajawahi kuolewa kabisa)
Vigezo vilivyopitiliza viwango (hasa kwa
muonekano)
Wanawake wengi hasa wa umri mdogo
(lakini unatosha kuolewa) hutumia muda
mwingi katika kuchagua aina ya
mwanaume ambaye angependa awe
mume wake.Wanawake hawa hujiamini
zaidi na kusimamia sifa zile ambazo
huamini ni muhimu mwanaume wa
kumuoa awe nazo.
Vigezo hivyo huwa hata kwa misingi ya
muonekano wa mwanaume huyo – kuna
wale ambao hutaka mwanaume huyo wa
kumuoa awe na sifa kama vile, mrefu,
aliyejazia kifua, mtanashati, sauti nzuri n.k.
Inaweza kuwa kama mzaha na ikaonekana
ni kipengele kidogo sana lakini bado kuna
wale ambao anaweza kuwa tayari kuolewa
ila hataki sababu tu huyo mwanaume
hafananii vile ambavyo yeye anataka
mumewe awe.
Kutaka mwanaume tajiri
Kuna wanawake ambao tayari
wameshajiwekea akilini kuwa hatakubali
kuolewa na mwanaume yeyote yule
ambaye hana pesa nyingi.
Yupo tayari kuolewa ila si kwa mwanaume
mwenye uwezo wa kawaida – hata
ikitokea mwanaume ana uwezo kidogo wa
kuweza kujitosheleza, yeye bado huona
huyo mwanaume hamfai hadi pale tu
atakapo pata yule ambaye anahisi ataishi
maisha ya kifahari.
Hivyo hukazana kusubiri na kujitahidi
kuwinda aina ya mwanaume ambaye
atakuwa na uwezo mkubwa, bila kujalisha
kama huyo mwanaume kampita sana umri.
Kutompata Mwanaume Ampendae
Hili ni kama tu vile ilivyo kwa wanaume
ambao huamini ndoa haiwezekani na
haifai bali tu hadi pale umpatapo yule
ambaye unampenda na unaamini
anakupenda pia.
Wengi katika kundi hili huamini kuwa
mafanikio ya ndoa kigezo kikubwa ni
kupendana tu na mengine hufuata kwenye
sababu ya upendo. Kunawanawake vigezo
vya mwanamme awe vipi havina umuhimu
kabisa katika kutaka kuamua kuolewa.
Yeye kikubwa anataka ampate mume
ambaye atampenda kwa dhati na huku
akiwa na matumaini kuwa huyo mume
atampenda na yeye pia kwa dhati. Huyu
mwanamke anaamini msingi bora wa ndoa
ni mapenzi ya dhati kati ya yeye na mmewe
basi! Hana haraka hadi pale atakapompata
mwanaume akampenda ndipo
atakapokuwa tayari kuolewa.
Kuchagua mno Wanaume wa Kumuoa (SO
SELECTIVE)
Kuna wale wachache ambao akili
hubadilika kama kinyonga; wasioridhika
wala kujitambua ni nini wanataka ama
mwanaume wa aina ipi wanataka.
Akija wa mwenye uwezo atasema nataka
wa kuchuma nae, akija asiye na uwezo
atatoa sababu tu hata kama kumlaumu
kuwa inaonyesha hajitumi kutafuta
maendeleo.
Akija wa kabila hii, atasema hapana hao
wana tabia hii mimi siitaki! Yaani kwa ufupi
ni mtu asiyeisha kutoa kasoro za wale
ambao wanajitokeza kutaka kumuoa.
Hatimaye inaweza tokea muda wa kuolewa
ukapita na akaishia kupunguza
uchunguzaji lakini ikiwa hata wanaume wa
umri wa kufaa kumuoa kutokuwepo tena
katika soko.
Kujiona ni mzuri sana
Kuna wanawake ambao ni kweli Mwenyezi
Mungu kawajaalia uzuri hasa (uzuri wa
muonekano), anakuwa ni mzuri kiasi
kwamba wake kwa waume wote
wanamkubali kwa uzuri huo na hata wote
kumtamani.
Hata hivyo hapo hapo kuna wale ambao
huwa ni wazuri kawaida – ila kwa
mtazamowake hujiona ni mzuri mno
hakuna mfano kama yeye; kitendo
ambacho kwa wachache kwenye kundi hili
hufanya kujiona yeye ni yeye na kuwa kwa
yeyote kuwa na yeye huyo mtu anatakiwa
atambue kuwa ana bahati sana.
Kitendo hiki hukuza nyodo za hali ya juu ya
mwanamke mwenye mtazamo huu, kiasi
kwamba wanapojitokeza wanaume kutaka
kuoa – anaweza onyesha tabia kama
maringo, dharau na kiburi.
kujiona ana Umri mdogo
Binti yeyote wa miaka 18 na kuendelea
anaruhusiwa kuolewa endapo tu karidhia
kuolewa.
Wanawake wametofautiana mipangilio yao
ya kimaisha, kuna wale akiwa katika umri
wa kuolewa hutamani sana kuolewa na
kuna wale ambao hupenda kuolewa
wakiwa wakubwa zaidi.
Katika kundi hili umri kuwa mdogo
hutegemeana, kuna mwingine anakuwa na
umri wa miaka 25 na bado akajiona
mdogo na hali kuna mwingine anakuwa na
miaka 20 na akajiona ni mkubwa na anafaa
kuolewa.
Hii pia ni kwa wanawake wale ambao
huwa na malengo ya kutotaka kuharakisha
katika ndoa.
Anapokuwa na umri ambao anaweza
kuolewa lakini yeye hayupo tayari kwa
muda huo, huwa ni kikwazo kwake kuingia
katika ndoa.
Maradhi hasa UKIMWI
Hili kama lilivyo kwa wanaume - Pamoja na
kuhamasishwa kwingi na wataalamu wa
maradhi ya HIV/AIDS kuwa mtu hata ukiwa
umeathirika unaweza kuwa na mahusiano
na hata kuoa na kuwa na watoto; bado
haisaidii sana kwa vijana wanaojitambua
kuwa ni waathirika wakiwa bado ni
wadogo, hawajaoa/olewa ama kuwahi
kuwa na mtoto.
Wengi sana hukata tamaa na huona ni
kheri kubaki walivyo kuliko kuingia katika
ndoa, hasa tokana na imani kuwa
wanawake wakizaa wakati ni waathirika;
afya hudhoofika zaidi.
Kutaka maisha ya Tamthilia (Ndoa za kuishi
kwa furaha milele)
Kutokana na kukua kwa idadi ya tamthilia
nyingi ambazo huonyesha maisha ya
kimagharibi zaidi; kumekuwa na dhana
kwa baadhi ya wanawake kutaka hayo
maisha ya tamthilia yawe na kwao pia.
Hilo linafanya vigezo ambavyo mwanamke
huyo anatumia kuchagua ama kukubali
mwanaume kumuoa kutotimiza yale
ambayo yeye binafsi anatarajia.
Wengi hushindwa kutambua kuwa hakuna
maisha ya furaha milele, na hasa kuwa
maisha ya maigizo yapaswa kuchanganya
na zako kuweza kufanya maamuzi ya kipi
kiigwe na kipi kiachwe kama kilivyo.
Kuona taasisi ya Ndoa kama Utumwa
Mtazamo huu kwa wanawake wenye
msimamo huu, huchangiwa na baadhi
kama haya:
- Usomi: Aina ya usomi ambao hupelekea
kwa baadhi kuwa na tafsiri tofauti juu ya
ndoa, haki, majukumu na mengine mengi.
- Kushuhudia ndoa mbovu: Hii inaweza
kuwa ya wazazi/walezi wake wenyewe
(pengine mama aliteswa sana), na hata
ndugu wa karibu kama vile kushuhudia kila
ndoa ya ndugu yake anayoijua mwanamke
huishi kwa mateso, manyanyaso na maisha
ya taabu na kuonewa.
- Kuwa na uwezo sana wa kujitosheleza
ambao unaweza kumtimizia na kufanya
lolote lile ambalo anataka katika maisha.
Kwake kuwa na mwanaume kama mume
kwake anaona kama ni utumwa.
Kutokuwa kabisa na mshipa wa hisia za
kufanya mapenzi
Kuna wanawake wale wachache
waliozaliwa hivyo. Hawana hisia yoyote ile
ya kimwili ya kuweza kupata hisia za
kuweza kujisikia ama kutamani kufanya
mapenzi.
Wengi wa aina hii ya wanawake huwa ni
waoga sana wa kuwa karibu na
mwanaume, na kwa wale ambao
wamewahi hata jaribu baadhi huona kama
kitendo cha ndoa ni kero, unyanyasaji na
uchafu.
Hivyo wazo la kuwa akiolewa anatarajia
kufanya kitendo cha ndoa mara kwa mara
kinamvunja kabisa hamu ya kutaka
kuolewa.