Nimekaa sehemu leo napata lunch, mara
dada mmoja mrembo aliyekuwa karibu
yangu "kareact", "mameseji kibao halafu
marefu, hayaeleweki.
Unanijazia tu inbox, utakuwa masikini tu
sana. Baada ya dakika kama 2 hivi..
nikamuuliza dada yangu mbona hasira
sana, kwa nini.
Akanijibu "kuna jianaume linanijazia tu
inbox, linatuma messages nyingi, ndefu
halafu halieleweki, wiki ya pili sasa, mie
ananiudhi!"
Nikamwuuliza "mbona unasema atakuwa
masikini,akajibu "mtu mwenye hela zake
na anayejiamini atahangaika kutuma
mameseji kibao, marefu ambayo hata
hayaeleweki."
Kwani huyo hawezi kuwa tajiri, lakini
kumbe anafanya ufafanuzi kwa kuandika
kwa kina,"ingawa simjui, atakuwa hana
lolote, anafikiri akijieleza au kuandika sana
nitamhurumia au nitamwelewa, akafie
mbele huko, tena namblock, hii ni kawaida
ya wanaume kapuku."