Monday 11 May 2015

AMESOMESHWA KUANZIA KIDATO CHA KWANZA HADI CHUO NA MWANAMKE, KUNUNULIWA GARI, SASA HIVI ANAMUONA MWANAUME MSHAMBA NA ASIYEKUWA NA HADHI YA KUWA NAYE SI KATIKA MATEMBEZI WALA KUMPA PENZI KAMA ZAMANI.


Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 28 Naishi Tabata jijini Dar Es Salaam nimejitokeza kwenu kuomba ushauri, Mimi na mpenzi wangu ambae amenisomesha toka form one hadi sasanipo chuo kwani wazazi wangu walifariki wakati mimi nikiwa mtoto mdogo sana.Sasa huyu mpenzi wangu amenigharamia sana yani kuanzia nguo zote hadi chakula nacho kula vyote ni msaada wake yeye na amejitolea kuninunulia gari la kutembelea na kanambia nitafute kiwanja ili tujenge nyumba ya kupangisha.Ila mimi kwa sasa naona kama huyu mwanaume hatuendani kwani yeye hana elimu ila anafanya kazi kutumia akili ya kuzaliwa, Jamani mimi nataka kuishi na msomi mwenzangu ila huyu kaka mimi naona kama freemasson kwani kanisaidia sana asije akanitoa kafala, Mimi kwa sasa nimepata mpenzi mpya ambae anaelimu ya chuo pia ni sharo sio mshamba kama huyu wa zamani.Sasa please naombeni ushauri wenu jamani nimwambiaje kama sipo tayari kuishi na yeye huyu mpenzi wa zamani bila kuumiza moyo wake...?