Rapa kutoka kundi la LaFamila, Chid Benz ametoa ufafanuzi wa kukamatwa kwake siku ya Agosti 12 mwaka huu baada ya kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroine.
Chid amekanusha vikali tuhuma hizo kupitia E-Newz ya EATV na kusema kuwa stori hizo zinatengenezwa na washindani wake ili kumharibia kimuziki.