Tuesday 29 August 2017

Kiba Aonyesha Jeuri Mbele ya Diamond Seduce Me Yagonga Views Milioni 2 Ndani ya Siku 3

Msanii wa Bongo Flava, Alikiba amezidi kuweka rekodi kupitia wimbo wake mpya ‘Seduce Me’ ambapo kwa sasa umefikisha views Milioni 2 ndani siku tatu.

Hapo awali wimbo huo uliweka redodi ya kufikisha views milioni 1 ndani ya saa 37 sawa na siku moja na masaa 13 na kuweka rekodi ya video iliyotazamwa zaidi kwa muda mfupi Tanzania na Afrika Afrika mashariki kwa ujumla, hivyo kuipuku video ya wimbo wa Salome ya Diamond iliyotazamwa na watu milioni 1 kwa siku mbili.

Kwa sasa video inayoongoza kushikilia rekodi ya kutazamwa zaidi kwa muda mfupi barani Afrika baada ya kutoka ni Video ya Closer ya Wizkid ambayo ilitazamwa na watu milioni 1 kwa masaa 23.