Tuesday 29 August 2017

Lulu Michael Ampiga Dongo Babu Kubwa Diamond Baada ya Kutoa Wimbo ili Auzime wa Ali Kiba

Mrembo kutoka kiwanda cha filamu Bongo, Elizabeth Micheal maarufu Lulu ameamua kutupa jiwe gizani katika mtandao wa kijamii wa Twitter ambapo ameandika umeshagundua kitu kizuri ukikifanya kwa nia mbaya hakifanikiwi kwa uzuri wote.

Kupitia mtandao huo Lulu ameandika “Hivi Umeshagundua Kitu Kizuri Ukikifanya kwa Nia Mbaya Hakifanikiwi Na Uzuri wake woooooote…!😒.”


Kauli ya mrembo huyo imetafisiriwa kuwa ni ndogo kwa WCB, baada ya kuachia ngoma siku sawa na Alikiba, kitendo ambacho ngoma ya Alikiba imeonyesha ikiwa na kasi ya kupata views wengi na kutreanding kwa muda mrefu.