Thursday 31 August 2017

Emirates yafanya Uteuzi wa Meneja Mkuu Mpya kwa Tanzania

Emirates imetangaza uteuzi wa Mheshimiwa Rashed Alfajeer kuwa meneja mkuu mpya nchini Tanzania.

Bwana Alfajeer, kutoka katika nchi za kitaifa wa Falme za Kiarabu, atakuwa na jukumu la kusimamia shughuli zote za emirates za kibiashara, wateja na mizigo kwenye soko.

"Nina furaha kwa kuchaguliwa kuwa meneja mpya wa Emirates nchini Tanzania na ninatarajia kufanya kazi na timu ya ndani, pamoja na washirika wetu wa biashara katika kuendeleza biashara zaidi ya Emirates kwenye soko," alisema Alfajeer.

"Mtazamo wangu utakuwa kuendelea kuwapa wateja wetu wa Tanzania huduma bora kulingana na thamani ya pesa, tunapowaunganisha kwenye maeneo zaidi ya 150 ulimwenguni kote," aliongeza.

Bwana Alfajeer alijiunga na Emirates mwaka 2013 kama sehemu ya mpango wa Emirates kama msimamizi wa Taifa wa Uendeshaji wa Biashara. Tangu wakati huo, amefanya kazi za biashara nchini Sri Lanka kabla ya kuchukua nafasi ya Meneja wa Wilaya huko Dammam, Saudi Arabia mwaka 2015.