Monday 25 September 2017

Wachina wasepa na ngoma za Mrisho Mpoto

Ngoma ambazo zilikuwa zinatumiwa na msanii wa muziki wa asili, Mrisho Mpoto katika maonyesha ya Utalii Duniani yaliyofanyikia nchini China zimegombaniwa na baadhi ya wachina waliojitokeza katika maonyesho hayo. 


Mpoto amesema ngoma hizo ziliwavutia wadau wengi ambao walijitokeza katika maonyesha hayo kutokana na namna ambavyo zilikuwa zinapigwa. 


Pia muimbaji huyo katika maonyesho hayo alipata fursa ya kutoa elimu kwa wachina hao kuhusu utalii wa ndani.