Tuesday 15 July 2014

HUYU DEMU MCHARUKO DAR NZIMA SIJAPATA KUONA TAZAMA VIMBWANGA VYAKE


 
Haikupita ‘taimu’ kwani mzazi huyo alipotelewa na uungwana pale alipojikuta akisimama na kuanza kuserebuka sambamba na mwanaye.


Kadri mapigo ya Vijana wa Masauti yalivyozidi kuchanganya, ndivyo midadi ya ‘mtu mzima’ ilivyozidi kupanda na kuanza kukata kiuno isivyo kawaida huku akichojoa kiwalo kimoja baada ya kingine.

...mzuka wangu ukinipanda......

Mzuka ulipokolea barabara, mama alijikuta akivua miwani yake ‘tintedi’ kwani ilikuwa ikimnyima raha kwa kutoona vizuri kwenye giza.

Baada ya miwani vilifuatia viatu, blauzi na kubakiza sidiria, huku chini akishusha ‘skini jinsi’ yake na kusababisha bikini na viungo nyeti kuwa nje nje mbele ya mwanaye aliyekuwa akiangalia pembeni kwa aibu kuu.

...hata nguo huwa navua...!

Mizuka ya mama huyo ilishindwa kutulizwa mpaka wasamaria walipoamrisha Vijana wa Masauti kuzima muziki ndipo mzazi huyo akatulia na kwenda kukaa huku watu wakimponda kwa kitendo chake cha kumwaga radhi mbele ya mwanaye. Baadaye alitimkia kusikojulikana huku mtoto akielekeza njia tofauti na walipoingia kwani mama ndiye aliyekuwa ‘dairekta’.