Wednesday 25 October 2017

SIMULIZI: DADA VUA 13


..........ilipoishia

Huku kwa kina Helena tayari Lucy alisharejea katika hali yake ya kibinadamu na wakati huohuo Sule alionekana anaondoka.Kwa kuwa helena alikuwa amepewa kazi ya kumzuia sule asiondoke bila kunywa kinywaji kile alichopewa na Shangazi,Basi alimfuata sule akiwa na kile kinywaji kujaribu kama hilo litawezekana.....

Basi Helena aliutumia tena usichana wake kumshawishi Sule anywe kinywaji kile.Basi helena alimfuata sule mpaka alipo kisha akamwambia"sule naomba unisamehe mimi pamoja na shangazi yangu,Na pia shangazi kasema haina haja ya wewe kuondoka kwani umeshakuwa mtu wa karibu katika familia yetu".Sule alimtazama kwa umakini kisha akajiuliza,"Mmmmmh!! inawezekana vipi shangazi anifume na wote hawa na bado aniambie nimekuwa mwana familia!!?" Sule kwa akili yake fupi aliwaza kisha akagundua kuwa shangazi alikuwa anamchora pengine anamuitia polisi.Helena hakuishia hapo alizidi kuingea"Aaaamh! na pia kama umeamua kuondoka basi chukua kinywaji hiki kunywa ili uendako usinisahau".Sule alipokea kikombe kile kikiwa na kinywaji ndani tayari kabisa kwa kunywa.

Sule alishangaa kuona helena anabembeleza sana ili anywe kinywaji hicho.Sule machale yalimcheza akamrudishie helena kile kikombe na hakutaka kunywa kabisa"Helena pleas siwezi kunywa kinywaji hiki"........"Sule inamaana hunipendi kabisa babaaa!! mbona yale yashapita jamouny"........Sule taaratibu maneno ya mtoto wa kike yalianza kumuingia lakini nafsi yake ikawa na mashaka kwani mazingira anayopewa hicho kinywaji yalimpa hofu sule alijiuliza"Sasa kwa nini wasinipe wakati ule nilipokuja saizi nataka kuondoka ndio wanipe!! hapana hapa kuna kamchezo"Sule aliangalia kwa mbali alimuona Lucy na shangazi yake wakitazama jinsi anavyopewa kinywaji kile na bidada helena,Na hapo ndipo Sule alipoghairi kabisa swala la yeye kunywa hicho kinywaji.

HUKU NYUMBANI ALIPO MAMA YAKE SULE MAMBO YALIKUWA HIVI,

Mama yake sule baada ya kuona anakabidhiwa nyaraka na hati miliki za mali zao alianza kuingiwa na tamaa.Alitoa nje na kuanza kuzitazama gari zilivyopark pamoja na nyumba ilivyo nzuri,Aliangalia huku akionekana kama kuna jambo analitafakari kichwani.Mama yake sule aliingia ndani kisha akachukua simu yake na kuanza kutafuta namba,Alipofika kwenye namba ya Bi kidako aliitazama huku akionekana kujishauri kuipiga,Lakini aliikaza roho na kupiga.

"Haloo!! shikamoo bibi!!?"

📲marhaba mwanangu habari zenu huko

"Hatujambo kabisa vipi kuhusu swala la sule?"

📲Sule niko naye hapa ndio nafanya mpango jinsi ya kumfanya arudi

"Ooooooh!! ahsante sana kumbe tayari uko naye sasa tutampata vipi"

📲Atakuja usiku huu huu haitafika saa nne

"Sasa bibi naomba unisaidie kitu"Mama yake sule aliongea huku akipepesa macho kuangalia kama yuko mwenyewe.Aligundua kuwa yuko mwenyewe na ndipo alipomwambia maneno haya bi kidako.

📲 sema tuu mwanangu

"Aaaamh!! unajua mi sitaki kabisa kuishi na huyu mwanaume na nataka ufanye jambo hapo"

📲 kwa hiyo wataka tufanye nini?

"Kesho anasafiri sasa nataka akienda huko iwe ndio mwisho kuiona tanzania na ukikubali kunifanyia hivyo nitakupatia milioni 20 kama zawadi na nitakujengea nyumba nzuri hapa mjini kama utataka ila kama utataka huko huko pia sawa"

📲Sawa lakini ni ngumu sana ila nitajitahidi lakini uwe makini sana kwani ni hatari,Nitafanya hivyo lakini nakusihi tena kuwa makini na naomba akishaondoka tuu ukuje huku na pia chakula cha wanao kimekwisha uje nacho.

"Yaani nitashukuru sana kama hilo jambo litafanikiwa sasa mimi kesho nakuja huko lakini hakikisha sule aje huku leo ili kesho tufanye hii niliyokuambia"

Yaani hapa wamekutana Mganga ana tamaa na mama yake sule ndio balaa.Walikubaliana kisha mama yake sule alikata simu,Wakati anageuka tuu alikutana uso kwa uso na kijana wake Wedi,Mama alishtuka sana alionekana kama ana wasiwasi kutokana na kile alichokuwa anazungumza kwenye simu.Alivuta pumzi kisha akaongea"Hujambo mwanangu??"......Wedi alimjibu"Yaani mama una bahati nilikuwa nije nikufumbe macho sema umewahi kugeuka"Wedi aliongea kisha akanyanyua funguo ya gari juu huku akimwambia mama yake"Supriseee!!!!!"......"Mama alishangaa sana"Whaaat!!"....Wedi alimwambia"Njoo uone huku nje.Mama alivyotoka nje alishangaa kukuta gari 2 zimepark nje moja ina plat namba imeandikwa MAMA na nyingine imeandikwa BABA.

Wakati huo mzee alikuwa ndani anajiandaa andaa kwa ajili ya safari yake.Mama alipigwa butwaa kwani ni jambo linaloshtua sana kitendo cha watoto kuwapa magari sio kitendo kidogo.Wakati wanashangaa mara sudi alitoka ndani akiwa amemziba baba yake macho mzee alikuwa anaongea ongea huku anacheka"Halafu nyie watoto mna masihala mjue huuhuuhu!! angalia usinigongeze mlangoni oohooo!!"Sudi aliwaambia"Shiiiiiii!!"Yaani wanyamaze kisha akampeleka mpaka pale mbele ya gari na kumwambia "Ebu papasa hapo" Mzee alipoligusa tuu lile gari na Sudi akamuachia macho,Basi mzee aliangalia kisha Sudi akamkabdhi ufunguo huku akisema"Tumefurahi sana kitendo cha nyie kuona umuhimu wetu hasa hasa mama kwani bila yeye nahisi usingewaza kutufanyia hivi baba yetu,Na tumeona tufanye hivi kabla haujasafiri baba yetu".Basi ilikuwa ni furaha kubwa kwenye familia ile,Kwanza walipiga picha nyingi mno mavinywaji nyalitolewa ndani walikunywa na mpaka basi.

Upande wa pili kule Sule aligomea kabisa kunywa kinywaji cha Helena.Sule alimwambia"Mbona unaning'ang'aniza sana kwanza sitaki hicho kinywaji hata wewe pia sikutaki tena"Sule aliongea kwa hasira kisha akawa anaondoka.Shangazi yake Helena alikuwa kwa mbali anatazama,Alivyoona sule amekataa alisema "Ahaaaaa!! unajifanya mjuaji eeeeh!! ngoja nikuonyeshe adabu" Aliongea huku akiingia ndani...........Nini kitafuata?? usikose sehemu inayofuata.