Sunday 22 October 2017

Nape Nnauye afunguka tena

Mbunge wa Mtama, kwa tiketi ya (CCM) Nape Moses Nnauye amefunguka na kuwataka watu kuacha ushamba kwani kusifu au kukosoa juu ya jambo fulani ni kazi ambazo Mungu amewapa watu kuzifanya hivyo mtu baki hupaswi kukerwa na kuhangaika na hayo.

Nape Nnauye amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter na kusema mtu ambaye anachukizwa na watu ambao wana sifu juu ya jambo fulani au kukosoa basi huyo mtu ni mshamba.
"Mungu kagawanya kazi, wengine kusifu, wengine kukosoa, wengine yote pamoja! Kwanini unakerwa na kuhangaika na mgawanyo wa kazi? !Acha ushamba" alisistiza Nape Nnauye
Aidha kiongozi huyo amezidi kusisitiza kuwa watu wanapaswa kutimiza wajibu wao na kuacha kuhangaika na watu ambao wanasifia juu ya mambo au kukosoa.