Tuesday 24 October 2017

Nay wa Mitego amjia juu mtayarishaji

Msanii Nay wa Mitego amesema kitendo cha Daxo Chali kuwafukuza kwenye lebo ya Mj Record wasanii wake Nini na Haytham kwa kosa la kuwa na mahusiano na mmoja kati yao, ni kitendo cha kipuuzi.

Nay wa Mitego ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kwamba jambo hilo haliingi akilini na inadhihirisha upuuzi uliopitiliza.

Pamoja na hayo Nay wa Mitego ametoa ushauri kwa kiongozi wa lebo hiyo ambaye ni producer mkongwe bongo Master Jay, kuangalia usimamiaji wa lebo hiyo kwani vitendo vinavyotokea vinaitia doa.