Thursday 27 July 2017

Ruby amuonyesha baba kijacho

Baada ya kumfichaficha mwandani wake ambaye anadaiwa kumpa ujauzito msanii wa Bongo Fleva, Ruby ameamua kuonyesha rasmi sura ya mwanaume huyo.

Picha ya mwanaume anayedaiwa kuwa mpenzi wa Ruby

Kupitia mtandao wa Instagram, Ruby amempost mwanaume huyo mwenye asili ya kiarabu ambaye anafahamika kama mwanamitindo na kuamuandikia maneno yaliyojaa na utamu huku akithibitisha kuwa ndiye baba kijacho wake.

“My prince charm,my smile maker ,BABA PRINCESRUBY ,” ameandika mrembo huyo. Kwa muda wa wiki kadhaa mkali huyo wa ngoma ya’Kwikwi’ amekuwa akidhaniwa kuwa ni mjamzito kutokana na picha anazopost katika mitandao ya kijamii.