Wednesday 26 July 2017

Country Boy ataja sababu ya kufananishwa na Young Lunya

Msanii wa muziki Bongo, Country Boy ametaja sababu za rapper Young Lunya wa OMG ambaye ni mdogo wake kufananishwa naye.


Akiongea katika Planet Bongo ya EA Radio, mkali huyo ya ‘Trurn Up’ ameeleza kuwa mkali huyo amekuwa akisound kama yeye ila kwa baadhi ya sehemu ndio anakuwa hivyo.

“Young Lunya kwanza ni mdogo wangu sema wakati anataka kutoka alikuwa anasema mimi na yeye, yeye ni mkali.. nikamwambia bro chill out bhana nitakufundisha njia za kutoka, hata Mwana FA anajua nini, ila kuna time nikimsikiliza najiona mimi kabisa,” ameongea Country.