Wednesday 26 July 2017

Celine Dion akanusha kutoka na ki-Ben10

Mwanamuziki mkongwe dunian, Celine Dion(49) amepinga vikali tetesi zinazodai kuwa anatoka kimapenzi na mcheza dansi wake Pepe Munoz(32).

Celin Diaon na Pepe Munoz wakiwa matembezini Paris -Ufaransa

Celine ambaye alifiwa na mumewe Rene Angelil, mnano mwaka 2016 Januari amekanusha tuhuma hizo kupitia mtu wake wa karibu baada ya picha zake akiwa na kijana huyo mjini Paris kuzagaa.

Kwa mujibu wa mtu huyo ameumbia mtandao wa TMZ, kuwa picha zilizagaa vikionyesha wawili hao wakiwa matembezini na wenye furaha na kufanya watu wajue kuwa ni wapenzi sio kweli bali ni watu wanaofanya kazi pamoja na Pepe amekuwa akitumika na Celion katika matamasha yake ya kimuziki , pia kijana huyo amekuwa na mchango mkubwa katika masuala ya mitindo.