Wednesday 31 May 2017

Upepo Mkali Kuvuma Dar, Wananchi Watakiwa Kuchukua Tahadhari..!!!

Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imetoa tahadhari ya upepo mkali na mawimbi makubwa katika maeneo ya ukanda wa pwani.


Taarifa ya TMA iliyotolewa jana imesema upepo huo unatarajiwa kuendelea hadi kesho.


Maeneo yanayotarajiwa kuathirika ni mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam, Tanga, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.


Mamlaka imesema hali hiyo inatokana na msukumo wa upepo wa kusi unaotokana na kuimarika kwa mgandamizo mkubwa wa hewa katika ukanda wa pwani ya Tanzania. TMA imetoa angalizo kwa watumiaji wa bahari na wakazi wa maeneo hayo kuchukua tahadhari na hatua stahiki