Wednesday 31 May 2017

Nani amemsnitch Diamond? ‘Too many fake people in this world’

Nani amemvuruga Diamond? Mkali huyo wa wimbo ‘Mary You’ ametuma ujumbe mtandaoni kuonyesha kuna kitu hakipo sawa miongoni mwa watu wanaomzunguka.

Diamond Platnumz

Muimbaji huyo kwa sasa yupo nchini Uganda kwaajili ya mazishi ya aliyekuwa mume wa zamani wa Zari, Ivan Ssemwanga aliyefariki wiki iliyopita nchini Afrika Kusini alipokuwa alitibiwa matatizo ya moyo.

Bosi huyo wa WCB amepost picha yenye ujumbe ‘Too many fake people in this world’ kauli ambao imezua gumzo mitandaoni huku baadhi ya watu wakidai ni dongo kwenda kwa mtu wake wa karibu aliyemzingua.


Ujumbe huo haukujulikana moja kwa moja unaenda kwa nani kutokana muimbaji huyo kutoonyesha kama ana ugomvi na mtu yoyote.

Baadhi ya mashabiki katika mitandao ya kijamii wameonyesha kuachwa njia panda na post hiyo licha ya baadhi yao kumuunga mkono kwamba ni kweli kuna watu ‘fake’