Wednesday 31 May 2017

Kesi ya ulevi ya mkalia kooni Tiger Woods

Siku moja baada ya mchezaji nyota wa gofu Tiger Woods, kukanusha kuwa hakuwa amelewa wakati polisi walipomkamata siku ya Jumatatu, taarifa za polisi zinasema kuwa mchezaji huyo alikutwa amelala ama (amezima) kwa ulevi wakati injini ya gari ikiwa inafanya kazi.

Mchezaji nyota wa gofu Tiger Woods

Mchezaji huyo aliyekuwa akishikilia nafasi ya kwanza katika viwango vya ubora duniani, alikutwa katika usukani wa gari yake aina ya Mercedes na aliamshwa kwa dakika kadhaa na afisa wa polisi aliyemuona.

Tiger Woods, alikamatwa kwa kosa la kuendesha chombo cha moto akiwa amelewa lakini alikanusha hilo na kusema kuwa ni matokeo ya dawa kali anazozitumia baada ya kufanyiwa upasuaji wa mgongo.