Tuesday 30 May 2017

Kijana Unapoamua Kuoa Mwanamke Mrembo, Msomi au Binti wa Kidigital Basi Kubaliana na Haya...!!!


Vijana wenzangu unapoamua kuoa mrembo, msomi na binti wa digital, lazima ukubaliane na haya;
1. Wasichana wengi sasa hawajui kupika. Wanajifanya wamechoka nitanunua msosi sana tu, tena usipokaza hata chai ataenda kununua.


2. Usishangae nguo zako kutofuliwa wiki mbili, anaweza kumuita mdogo ake anamlipa afue. Yeye anachart sio na wewe ujue ni shotizo.


3. Kupiga deki sahau kijana mwenzangu. Aanze tu kupinda mgongo. Kama unataka usafi wa nyumba yako tafuta housegirl.


4. Jua kuwa utawahi wewe kuamka, yeye bado kalala. Amechoka kazi za ofisini za jana yake.


5. Bajet ya saloon iwepo ya kila wiki nywele na kucha.


Usilalamike ndo gharama za kufanya maamuzi hayo.