Tuesday 31 January 2017

Picha: Obama na mkewe wafurahia mapumziko British Virgin Islands na bilionea Richard Branson


Rais wa zamani wa Marekani, Barack Obama na mkewe Michelle wanaendelea na mapumziko yao huko British Virgin Islands, na Jumanne hii waliungana na mwenyeji wao, bilionea wa Uingereza, Richard Branson.


Obama na mkewe walisafiri kutoka Palm Springs walikokaa siku za wikiendi kwenda kwenye visiwa hivyo kwenye private jet ya Branson.


Wawili hao wanaaminika kuwa wamefikia kwenye moja ya visiwa vinavyomilikiwa na bilionea huyo.