Monday 30 January 2017

Gazeti la Mwana Halisi lapewa saa 24 liombe radhi


Gazeti la MwanaHALISI limepewa saa 24 kumwomba radhi Rais John Magufuli kutokana na kuchapisha habari iliyosomeka kwa kichwa cha, “Ufisadi ndani ya ofisi ya JPM.”




Mkurugenzi wa Idara Habari_MAELEZO, Hasan Abbas

Taarifa ya Idara ya Habari Maelezo iliyotolewa leo imesema habari hiyo iliyochapishwa katika toleo la Jumatatu, Januari 30-Februari 5, 2017, inajenga dhana kuwa Rais Magufuli anahusika na kilichoitwa ufisadi wakati msingi wa taarifa husika ni tatizo la manunuzi katika Shirika la Elimu Kibaha.

Hii taarifa yake: