Friday 23 January 2015

WEMA AJUTA KUWEKA KOPE BANDIA

BEAUTIFUL Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’ amefunguka kuwa anajuta kutumia kope za bandia kwa muda mrefu kwani zimeharibu kope zake za asili.

Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Wema alisema awali alikuwa hawezi kutoka kwenda kokote bila kuweka kope hizo na hata asipozibandika anajisikia vibaya lakini baada ya kumharibia muonekano wake wa asili, hataki hata kusikia.
“Jamani hakuna kitu ambacho nimekichukia kwa hivi sasa kama kope za

bandia sina tena ushawishi nazo kabisa zimeharibu macho yangu, situmii tena,” alisema Wema.