Friday 16 June 2017

Tunda Asanukia Ishu ya Kitumbo Chake Baada ya Kusemekana Mjamzito

Muuza nyago machachari Bongo, mwenye kupenda kujiselfisha akiwa kwenye maakuli, Tunda Sebastian amesanukia ishu iliyoenea kwamba, ana kibendi akisema kuwa kilichotokea ni mpangilio mbovu wa menyu ndiyo unamfanya aonekane tumbo hilooo!

Akibonga na 3 Tamu, amedai kuwa, kuna watu wanasema ana mimba, lakini hana cha mimba wala tumbo la mitungi bali ni mpangilio mbaya wa misosi.


“Sina mimba wala kitambi cha ulabu, hili tumbo limejaa misosi tu si kingine, kuna kipindi nilikuwa na mpangilio mbaya wa menyu. Najitahidi kufanya mazoezi na kupunguza kufakamia misosi,” alisema Tunda.