Thursday 29 June 2017

Wabunge Wanawake Watengewa Chumba Maalum cha Kunyonyeshea

Bunge limetenga chumba maalum kwa ajili ya wabunge wenye watoto wachanga kunyonyesha watoto wao wakati vipindi vya bunge vinaendelea.

Uamuzi huo umetangazwa leo (Jumatano) bungeni na Naibu Spika Dk Tulia Ackson mara baada ya kipindi cha maswali na majibu bungeni.

"Ofisi ya Bunge inataarifu kuwa imetenga chumba maalum kwa ajili ya kunyonyeshea kwa wabunge wenye watoto wachanga,"amesema.

Amewasihi wabunge wenye watoto wachanga kuwanyonyesha watoto wao angalau miaka miwili kama inavyoshauriwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto