Mtayarishaji wa muziki kutoka Touchez Sound, Mr Touchez amepigilia msumari tofauti zake na Nay wa Mitego kwa kusema hana alichopoteza kutoka kwake kwani hata kwenye show zake huwa haendi wala kuposti chochote kinachomuhusu.
Mr T Touch
Mr T- Touch amesema alinyanyaswa sana wakati yupo chini ya Lebo ya Nay wa Mitego ‘Free Nation’ kwani alikuwa anapoteza muda tuu hakuna kitu alikuwa anaingiza.
Mr T Touch kwa sasa yupo na Studio yake ya Touchez Sound na amesema mafanikio kwasasa anayaona tofauti na kipindi cha nyuma wakati yupo Free Nation.