Usaliti katika mapenzi unaumiza sana..kwa
nini inakuwa hivi?
Wanaume wengi wanapobaini kuwa
misuli kuonesha umwamba kwa
kuwatwanga makonde wapenzi wao au
kuwafanyia mbaya wale waliowanasa.
Lakini uchunguzi wa wana mapenzi
unaonesha kuwa ubabe haukomeshi tabia
ya usaliti.
Kuna wengi ambao waliwafumania wake
zao, wakawapiga na kuwajeruhi, lakini
wakajikuta hawakukomesha tatizo, zaidi ya
kuwapa usugu wapenzi wao wa
kuendeleza wizi tena kwa dharau na kejeli
huku wakibembelezana kwa maneno haya:
"mzushi kaenda kazini njoo sasa hivi
Wapendanao Gesti" au "vipi yule bwege
alikuuliza jana ulipochelewa kurudi" Jamaa
anaweza kumuuliza hivyo mke au mpenzi
wa mtu.
Katika hali ya kawaida usaliti ni jambo
linalouma kwa kiwango kikubwa. Katika
mapenzi hakuna suala la kuazimana mume/
mke. Watu huazimana magari na pesa,
lakini laazizi hakuna jasiri wa namna hiyo!
Hivyo ndivyo lakini, kupiga au kuachana
baada ya kufumaniana kunasaidia? Jibu
hakusaidii, kwani ukimpiga adhabu inaishia
hapo hapo, kesho yake watakaokutana
watakusaliti tena kupozana machungu.
Maamuzi ya kuacha naye hayasaidii kwani
ukimwacha mpenzi wako hujamtibu,
utakuwa umetoa mwanya wa yeye
kuendelea kukusaliti na kukuumiza zaidi
pale macho yako yatakapowaona
wameshikana mikono mitaani kwa uhuru
na raha zao.
Ukiamua kuua na wewe utauawa, huku
wanadamu wenzako wakikucheka kwa
uzembe wa kufikiri. Jamani usaliti upo kila
siku, si tunawaona wake na wapenzi wa
watu wanaingizana gesti kila siku?
Hivyo, kama hujamfuma mpenzi wako leo
kuna siku utakutana na meseji kali
akibembelezana na 'kidume' mwingine kwa
maeneo fulani. Utafanyaje baada ya kubaini
hivyo, maana kama ni tukio basi utakuwa
umeona lile la stejini laivuuuuuu bila
chenga. Twende pamoja ili tuelimishane
kama wadau wa mapenzi njia sahihi ya
kufanya ili kumwadhibu mpenzi msaliti.
Kwanza, baada ya kuwaona uso kwa
macho wakisaliti penzi, unatakiwa kutoa
ishara zitakazoonesha kuwa umewaona,
halafu ondoka eneo hilo. Ukifika home mtu
mzima endelea kunywa maji ili kupoza
presha. Akirudi mpenzi wako jitahidi
kumkaribisha kwa bashasha, lakini
usimuulize ulichoona mwache aendelee
kujiuliza mwenyewe.
Au kama umenasa meseji za kimahaba
kutoka
kwa mwizi wako, zitume kwenye simu yako
kwanza, kisha baada ya kumaliza
uchunguzi wako mtumie tena sms hizo
mkeo/mumeo. Ukifanya hivyo usimuulize,
endelea kumpenda na ikiwezekana ongeza
matunzo. Nunua 'mikuku' akaange kila siku
na umpe penzi moto moto.
Nakwambia ukifanya hivyo mpenzi wako
ataumia sana na hataendelea kukusaliti
kwa kuwa atakuwa anawaza unafikiria
kumfanya nini? Na kwa yule uliyemshika
naye, vivyo hivyo usizozane naye, mwache!
Utashangaa anahama eneo maana atakuwa
anafikiri unamwandalia kombora kumbe
wewe wala, umeamua kujituliza tu!
Wadau wa mapenzi hii ndiyo dawa ya mtu
msaliti. Mwadhibu kwa upole,
wanasaikolojia wameithibitisha adhabu hii
kuwa ina uchungu mara 1,000 zaidi ya
kupiga au kukemea. Ukisema umwache
siyo dawa kwani unaweza kutafuta
mwanamke/mwanaume mwingine naye
akawa na tabia zile zile, ikiwa ndivyo
utaacha wangapi basi katika maisha haya?
Adhabu ya mpenzi anayekusaliti ni
kumnasa kwenye usaliti wake kisha
kumpuuza huku wewe ukiendelea na
mambo yako kama kawaida, ukifanya hivyo
utakuwa unamtibu ugonjwa wake wa
kupenda penda hovyo na hii ndiyo dawa
hasa ya kumponya msaliti, lakini pia
inasaidia kupunguza maumivu ya penzi.
Kumchunga na kumlilia machozi hakusaidii.