Friday 29 August 2014

SAUZI KIMENUKA UCHUMBA WA MASOGANGE UMETIBULIWA MAMBO YAMEENDA MLAMA

SIKU chache baada ya kupata uraia wa Afrika Kusini, uchumba wa Video Queen, Agnes Gerald ‘Masogange’ na mpenzi wake, Louis Dolnard
umetibuliwa.
Video Queen, Agnes Gerald ‘Masogange’

Hali hiyo ilijiri kutokana na madai kuwa kuna wanaume wamepeleka maneno ya kimbeya kwa mpenzi wake huyo yakiashiria kuwa mrembo huyo hajatulia.
Hata hivyo, Agnes amefunguka kuwa kamwe hawezi kuachana na mchumba wake huyo.
“Wanaume wengine sijui wapoje, wanapeleka maneno ya kimbeya kwa mchumba wangu sijui wanataka nini? Kwa taarifa yao siachiki ng’o,” alisema Masogange.