Tuesday 26 August 2014

ASHA BOKO AIMBISHWA ‘TOILET’

Msanii maarufu wa komedi, Asha Mzuzuri maarufu kama Asha Boko, Alhamisi ya wiki iliyopita alinaswa na kamera yetu akiimbishwa na njemba eneo la choo cha wanawake ndani ya Ukumbi wa Mango Garden jijini Dar es Salaam siku ambayo
Mashauzi Classic ilikuwa ikitoa burudani.
Msanii maarufu wa komedi, Asha Mzuzuri maarufu kama Asha Boko akiwa na njemba eneo la choo cha wanawake.
Katika tukio hilo paparazi wetu aliwanasa wawili hao wakiwa kwenye maongezi huku wakijiachia kwa pozi za kimahaba na waliposhtukia kufotolewa waling’aka na kutishia kuharibu kamera.
Asha Boko akifurahia jambo na njemba hiyo.
“Hizi ni ishu zetu binafsi bwana, itakuwaje mtufuatilie mpaka chooni watu tushindwe hata kujiachia,” alisema Asha Boko, akichekacheka baada ya kubaini kubambwa.