Friday 22 August 2014

HAMISA APANGUA MSURURU WA WANAUME: MCHEPUKO SIO DILI

MODO maarufu Bongo, Hamisa Mabeto amekanusha vikali taarifa za kuwa ana msururu wa mabwana kama inavyosambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Modo maarufu Bongo, Hamisa Mabeto.

Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Hamisa alisema anawashangaa watu ambao wanamtaja kuwa na msururu wa wasanii ambao anafanya nao kazi wakiwemo wadau mbalimbali wa muziki kitu ambacho hakina ukweli wowote.
“Nazushiwa tu mara DJ Choka mara sijui nani, ni hivi sina mpenzi. Nikiwa na mpenzi kila kitu nitakiweka hadharani na kila Mtanzania atamjua,” alisema Hamisa.