Thursday 29 September 2016

ASIKWAMBIE MTU, HAKUNA TAMU BILA HAMU!

MARTHA MAGAWA
Kwa hili hata kidogo halitakiwi kufumbiwa macho, kwanini wasiojua maana ya ndoa wanawadhalilisha wanawake?
Wahenga walilitambua hili zamani, ndiyo maana msichana hakupewa ndoa mpaka apitie mafunzo kujitambua yeye ni nani ndani nyumba.

Kweli asiye na hamu hawezi kuiona tamu. Jamani kuolewa si mchezo wa kuigiza bali ni maisha yanayotambulika kihalali.
Unatakiwa kutambua kwamba ndoa ina raha yake hasa ukiijua, mumeo utamuona mfalme na wewe utakuwa malkia. Leo hii mtu anaolewa, hakai na mumewe zaidi ya kuzunguka kila kona, anakuwa kiguu na njia.
Inaoneka wazi hiyo ndoa yako umeolewa ili uonekane nawe umeolewa, lakini huna hamu nayo, siku zote kwako huioni tamu kwa sababu huna hamu nayo.
Mwenye kuwa na hamu na ndoa hawezi kukaa mbali na mumewe, wala kujichukulia madaraka mkononi, bali huikumbatia ndoa yake kwani hiyo ndiyo pingu ya maisha yake, kama hujawa na hamu na ndoa usiolewe. Hakuna tamu bila kuwa na hamu.