Wednesday 17 August 2016

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 21 & 22

Mtunzi:EDDAZARIA G.MSULWA
Madam Mery akaniwahi kunishika shati na kuanza kuniomba niache vurugu,mkuu wa shule akanyanyuka kwa hasira na kunisogelea na kunizaba kofi lililopelekea nikazidi kupadwa na hasira,Madam Mery akaendelea kuning’ang’ania kwa nguvu zake zote ila kutokana na nguvu nilizo nazo nikajitoa mikononi mwa madam Mery na kumfwata mkuu wa shule na kuanza kumrushia ngumi zisizo na idadi na uzuri zaidi kipindi nipo mdogo baba yangu alikuwa akinifundisha mbinu za kuweza kupigana kiasi kwamba hadi ninakua mkubwa swala zima la kupigana kwangu ni lakawaida.Waalimu wa kiume waliopo eneo la shule wakaja kutuzuia japo kuwa mkuu wa shule ni mzee kidogo ila na yeye alijitahidi kunipa makonde kadhaa yaliyo niingia vizuri sehemu mbali mbali za mwili wangu

“Eddy nakuomba uwe mpole kumbuka hapa tupo shule”
Madam Mery alizungumza kwa upole huku nikiondolewa eneo la tukio na waalimu wapatao wanne na kwajinsi nilivyo na nguvu na iliwalazimu kutumia nguvu nyingi katika kunizuia kwenda kuendeleza ogomvi na mkuu wa shule
“Wewe kijana mshenzi sana hujafunzwa huko kwenu hadi unapigana na mume wangu na nitahakikisha shule huna wewe mpumbavu mkubwa weee”

Mke wa mkuu wa shule alizungumza maneno yaliyozidi kunipandasha hasira laiti angejua mumewe kitu alicho toka kukifanya jana usiku wala asinge zungumza ujinga anao uzungumza
“Sawa waalimu wangu nimewaelewa ngoja mimi niondoke zangu naombeni muniachie”

Nilizungumza kwa upole na kuwafanya waalimu wa kiume walio nishika kuniachia taratibu na huku wakiniomba niondoke sehemu ya eneo la shule.Kwa haraka nikamsukuma mwalimu wa mbele yangu akaanguka chini nikapata nafasi ya kukimbilia eneo alilopo mkuu wa shule na nikamchomoa katikati ya watu wanao mpa pole na kumpiga kabali moja takatifu iliyotupeleka hadi chini ardhini na watoto wa mjini wenyewe tunaiita kabala ya mbao na kuwafanya walinzi na waalimu wa kiume kuanza kuushika mkono wangu na kuanza kuuvuta kwa nguvu ili kuyanusuru maisha ya mkuu wa shule.Wakafanikiwa kunichomoa huku mwili wangu ukiwa umejaa jasho jingi huku misuli ya mwili mzima ikiwa imetuna kiasi kwamba mtu aliyezoea kuniona kwenye mazingira ya kawaida atabisha kuniona kwenye hali ya hasira niliyo nayo sasa na atasema sio mimi

Mke wa mkuu wa shule akaanza kumfuta futa mumewe mchanga kwenye uso wake kiasi kwamba baadhi ya wanafunzi wakaanza kumcheka kwa jinsi anavyo tisha sura kwa kuchafuka.

“Oya Eddy tutakuchukulia hatua za kisheria sisi kama shule”
“Tea na wewe mwalimu wa nidhamu ninakumind kama nini sasa na wewe ingia kwenye kumi na nane zangu……Wewe unajua huu ugomvi umetokea wapi au unazungumza zungumza kumpa bichwa huyo choko wenu sifa……”
Nikasimama kwenye sehemu iliyopo juu na kuwafanya watu wote wanitazame kwa umakini huku wakinisikiliza akiwemo mkwe wa mkuu wa shule

“Huyo mzee wenu anahabari za kiseng* sana….Kazi yake ni kuwachukua wanafunzi wa kike na kwenda nao kwenye mahoteli makubwa na kufanya nao mapenzi.Ushahidi ninao na kama mwalimu yoyote atake bisha nitautuma kwenye wizara ya elimu tuone kama hii shule haito fungiwa”
Nilizungumza na kumuona Salome akijikatiza katikati ya wanafunzi na waalimu na kuja kupanda sehemu niliyo simama mimi huku akionekana kuwa na asira kali.Nikamtazama kwa jicho kali kiasi kwamba akatulia na kuzidi kuwafanya wanafunzi kuzidi kuongezeka wakitokea mabwenini na madarasani wakitaka kujua ni nini kinacho endelea

“Hapa nina gazeti linaelezea mambo ya huyo mzee aliyo yafanya jana usiku isitoshe alitaka kuniua kwa kunipiga na bastola ila kwa bahati mbaya akampiga mpenzi wangu na sasa hivi ninavyo zungumza amelazwa hospitalini”
Minong’ono ya wanafunzi ikaanza kutawala eneo tulilopo na nikaanza kazi ya kuwanyamazisha wanafunzi wezangu na kumfanya mkuu wa shule kuzidi kunitumbulia mimacho ya hasira na kila alipotaka kuondoka mke wake akawa anamzuia asiondoke

“Ngoja niwasomee habari ya hili gazeti na mukiwa amuamini nitawawekea video au picha za huyo mzee muone mambo mauvu anayo yafanya…….Kichwa cha habari cha hili gazeti kanasema HEAD MASTER AUA KISA MAPENZI habari ukurasa wa pili ianasema hivii….Mkuu wa shule moja jina tunalihifadhi anajiukuta akiangukia kwenye mikono ya polisi baada ya kumpiga risasi”

Nikapunguza sauti ya kulisoma gazeti kwani kitu kilicho andikwa kwenye gazeti kilianza kunichanganya kidogo na nikazidi kukisoma kimya kimya bila mtu kusikia
“Binti mmoja na kumuua kabisa.Muobgozaji wa filamu hiyo inayoitwa SCONGA LOVE imeshirikisha wasanii wengi maarufu kutoka nje na ndani ya mipaka ya Tanzania.Star wa filamu hiyo ambaye amecheza kama mkuu wa shule inasemekana ameweza kuziteka hisia za wasanii wezake alio wafanya nao kazi.Muandishi wetu alikutana na msanii huyo na mahojiano yalikuwa hivi”

Nikanyanyua macho yangu na kuwatazama wanafunzi na watu wengine wakisubiria niwasomee kilicho andikwa ndani ya gazeti hilo.Gafla sauti ya Salome ikaanza kusikika kwa sauti ya juu na kunifanya nimtazame

“Huu ndi mwisho wa manyanyaso ya wasichana wa kike kwenye hii shule…..Waalimu wengi hapa shule hututumia sisi kama vituliza nyeg* japo wana wake zao na wengine magirl friend zao……Mfano mzuri ni mimi.Jana asubuhi nilimuomba mwalimu wa zamu Pass(Ruhusa) ya kwenda kununua matumizi yangu binafsi kabla sijatoka getini mkuu wa shule akaomba anipe lipfti kwenye gari lake hadi mjini.Sikuwa na hiyana zaidi ya kukubali kutokana tumememzoea kama baba yetu wa kimwili na kiroho”

Salome alizungumza huku machozi yakimwagika na kunifanya na mimi niungane na wanafunzi wengine kumsikiliza kwa umakini wa hali ya juu
“Basi tukiwa ndani ya gari alipandisha vioo vyake vya gari lake na kuanza kunitongoza huku akidai atanipa kila nitakacho taka ikiwemo kunivujishia mitihani ya nusu mwaka kwa sisi A LEVEL……….Nilikataa na mwenzangu akazidi kuliendesha gari lake kwa kasi na sikuweza kushuka kwani hata mjini kwenyewe alinipitisha na tukafika kwenye moja ya hoteli na akanitolea bastola na kuniambia endapo nitakataa kushuka ndani ya gari ataniua.Sikuwa na ujanja zaidi ya kufanya kama alicho niagiza.Tukapitliza moja kwa moja kwenye chumba na head master akanilazimisha nifanye naye mapenzi bila kinga…….Na isitoshe aliniingilia kinyume na maumbile”

Mwili mzima ukafa ganzi nikabaki niemeduwaa huku wanafunzi wengie wakianza kutokwa na machozi wakimuonea haruma Salome.Ukelele mkali ukasikika katikati ya wanafunzi na ni mke wa mkuu wa shule alizidi kupiga makelela huku akiongea kichaga na kumpiga piga mumewe kwenye kifua

“Baba Evance mtoto wa watu umeshamuua wewe si unajijua kuwa sisi ni waadhirika ni kwanini sasa umefanya hivyo baba Evance”
Salome baada ya kuyasikia maneno ya mke wa mkuu wa shule akalegea mwili wake na kabla hajafika chini nikamnyaka na kumlaza taratibu na vilio vya wanafunzi wa kike vikaanza kutawala huku wengine wakidai wametembea na mzee huyo bila kinga na nimiongoni mwa wanafunzi walio ambukizwa virusi vya ukimwi.Waalimu wa kiume wakaanza kumchukua mwalimu mkuu na kumuingiza ndani ya gari la shule na wakaondoka kwa kasi katika eneo la shule kwani wanafunzi walianzisha vurugu za kuwarushia mawe

“NANI YUPO PAMOJA NAMI”
Wanafunzi karibia wote wakanyoosha vidole juu akiwemo rafiki yangu John ambaye alikuja wakati wa mwisho mwisho wa tukio na ninavyo mjua alikuwa ametoroka.Wanafuzni wakaanza kurusha mawe kwenye ofisi za waalimu na kuvunja vioo,nikamnyanyua Salome nikisaidiwa na wezake na tukamuingiza ndani ya gari langu huku John akiingia kwenye siti ya upande wangu huku akijichekesha chekesha.Nikawasha gari na kwa kasi ya hali ya juu nikanza kufwata njia ilipo elekea gari la shule kutokana katika eneo hiko kuna njia moja tu ya kutokea.Kwa mwendo kasi wa gari langu nikaanza kuliona gari alilopanda mkuu wa shule kwa mbali likikata kona kusoto kushika njia ya kuelekea porini kwenye migomba mingi

“Eddy na huyo Salome tunakwenda naye wapi?”
“Huko huko”
“Huko huko wapi akitufia mtoto wa watu itakuwaje?”
“Potelea pote ila cha msingi nilazima mkuu wa shule alipe kwa hili”
“Eddy mtu mwenyewe mbona kama haemi”
“John hembu niachie kelele”
Johnalizungumza kimasihara kiasi kwamba ninaona anazidi kunichanganya,Simu yangu mfukoni ikaanza kuita na ninamba ngeni ndio inayo ingia ikanilazimu kuipokea na kuweka loudspeaker
“Eddy mume wangu uko wapi?”
Ilikuwa ni sauti ya Sheila ikizungumza kwa upole
“Baby usijali ninakuja…hii namba ni ya nani?”
“Ni namba ya nesi nimemuomba”
“Umeshakula baby?”
“Ndio mume wangu……nakuomba ndani ya dakika kumi uwe umefika hapa la sivyo nitameza vidonge nijiue kabisa”
“Mke wangu usiseme hibyo”
“Nasema hivyo kutokana nina hamu na wewe na ninahisi upo na mwanamke mwengine”
“No baby naomba usinifikirie vibaaya”
“Sawa ila fanya hivyo nakuesabia dakika mume wangu”
“Sawa”

Nikakata simu na kuzidi kuongeza kasi ya gari langu hadi nikafanikiwa kulipita gari alilopo mwalimu mkuu kisha nikalisimamisha gari langu gafla kitendo kilichomfanya dereva wa gari alilopanda mwalim mkuu kunikwepa na kugonga mti mkubwa uliopo pembeni ya barabara nagari lao likasimama kiasi kwamba ndani ya dakika mbili hapakuwa na mtu yoyote aliye shuka kutoka ndani ya gari lao.Nikashuka na kuitoa simu yangu na kuanza kurekodi tukio moja baada ya jengine hadi ninafika kwenye gari la shule nikamkuta dereva wa gari hilo akiomba msaada wa kutolewa ndani ya gari hilo hii nibaada ya kubanwa na mskani wa gari kwenye kifua.Kitu kilicho nishagaza sikuweza kumuona mwalimu mkuu wala waalimu wengine wa kiume walio toroka eneo la shule

“Mkuu wa shule yupo wapi?”
“Ni…liwas…shusha…..njiani”
“Wapi?”
“Kul…e kwenye shamb…..a la migomba”
“Fuc*”
Nikamuacha derava akiendelea kubanwa na mskani wake na nikaingia ndani ya gari huku John akifwatia kwa nyuma na kuingia ndani ya gari na kufunga mkanda
“Eddy si tungemsaidia jamaa wa watu”
“Siwezi kusaidia mijitu mipumbavu kama yeye”
“Kwa nini?”
“Hii vita yeye haimuhusu kilicho mfanya aingilie ni nini?”
“Eddy kuwa na roho ya kibinadamu yule jamaa yupo powa sana huwa……”

“JOHN KAMA UNATAKA KUMSAIDIA SHUKA NDANI YA GARI LANGU NA UENDE UKAMSAIDIE”
Nilizungumza kwa sauti kali iliyo jaa hasira kiasi kwamba John akastuka na kukaa kimya,Nikageuza gari na kabla sijafika umbali kutoka lilipo gari la shule lilipo pata ajali nikasimamisha gari
“Eddy nishushe nikamsaidie jamaa wa watu”
“Powa shuka”
John akashuka ndani ya gari na mimi nikaendelea na safari ya kurudi mjini huku gari nikiliendesha kwa mwendao wa kasi ili nimuwahi Sheila aliye nipa dakika la sivyo anaweza kufanya kitu kibaya cha kujiua.Kitendo cha kufika hospitli nayo simu yangu ikaita kwa namba ile aliyo nipigia Sheila kwa mara ya kwanza nikaipokea
“Eddy mume wangu hutaki kuja eheee?”
“Nipo hapa nje”
“Kweli?”
“Ndio mke wangu”
“Sawa”

Nikamuita nesi mmoja na kumuonyesha Salome tuliye mlaza siti ya nyuma na kumuomba amtoe na kumfanyia huduma ya kwanza.Nikapitiliza moja kwa moja hadi chumba alicholazwa Sheila na kumkuta akiwa ana wasi wasi
“Baby mbona umechelewa”
Nikaanza kumuadisia Sheila kuanzia mwanzo wa tukio hadi mwisho wa tukio lilivyo tokea ila nilimficha juu ya uwepo wa Salome kwenye hospitali hiyo
“Sasa huyo mkuu wa shule yeye yupo wapi?”
“Sijui yupo wapi na mbaya zaidi jana alipo toka kufanya tulio la kukupiga risasi polisi wakamuachia huru”
“Mmmm mume wangu ninakuomba umpotezee”
“Siwezi kufanya hivyo yule mzee anatabia chafu na isitoshe anawaambukiza wanafunzi wa kike HIV kimakusudi”
“Weeee”

“Ndio hapa shule wanafunzi wengi wa kike nimewaacha wakili na nahisi ametembea na wengi sana”
“Mmmm kweli huyoo si mtu wa kuacha uraiani.Sasa wewe kama wewe umeamuaje?”
“Hi video nitaituma kwa mama kisha atajua nini cha kufanya”
“Ngoja kwanza ukimtumia mama yeye akikuuliza ulifwata nini hotelini utamjibuje?”
“Nitajua cha kumuambia mimi mama yangu hana neono”
“Mmm mimi ninakushauri usimtumie ni bora ukaituma kwa huyo waziri wa elimu”
“Umesha kula?”

“Ndio na wamenichoma sindano ya kukausha kidonda”
“Wamekuchomea wapi hiyo sindano”
“Kwenye makalio”
“Kwahiyo wamekushika mpododo?”
“Bwana Eddy hembu acha utani wako”
“Ngoja nikachukue msosi tangu jana tulipo kule njiani hadi sasa hivi sijaweka kitu mdomoni”
“Sawa mume waangu ila usichelewe kurudi”
Nikamnyonya lipsi Sheila na kutoka nje chumba na kwenda alipo lazwa SALOME na kukuta madaktari wakimshughulikia
“Dokta amepata tazizo gani?”
“Amepata mstuko wa moyo”
“Mmmm kwahiyo itakuwaje?”

“Ndio tunamshuhulikia kuurudisha moyo wake kwenye hali yake ya kawaida”
“Sawa dokta kila kitakocho endelea unijulishe kwenye hii namba”
“Sawa”Nikamuachia daktari namba yangu ya simu kisha nikatoka na kwenda kwenye mgahawa wa karibu na hospitali na nikaagiza chakula na kuanza kula taratibu huku nikitafakari ni nini nifanye juu ya ushaidi wa kumkamata mkuu wa shule.Tv(Luninga) iliyopo kwenye mgahawa Chaneli Ten ikaonyesha habari iliyo wafikia kwa wakati huo(BREAKING NEWS) na kunifanya niache kula na kuitazama kwa umakini.Nikashuhudia jinsi askari wakijitahidi kutuliza fujo zinazo endelea shuleni kwetu huku ofisi za waalimu zikiwa zinateketea kwa moto