Tuesday 16 August 2016

JE UKUBWA WA UUME NI JAMBO LA MUHIMU? SOMA HAPA

Je, ukubwa wa uume ni jambo la muhimu? Ni nini ukubwa wa uume mkubwa na Je wanaume wengi wana uume mkubwa? Haya ni baadhi ya maswali ambayo huzunguka katika baadhi ya akili za watu wengi. Kwa baadhi ya watu, uume mkubwa humfanya mtu kujiamini zaidi na kuongeza uwezo wa kumtosheleza mpenzi wake.


Jinsi ya kupima uume:
Kwa uume uliosimama kipimo ni kutoka chini ya uume unapokutana na mwili mpaka kwenye ncha ya uume. Kwa ya uume teke (uliolala) , pima mara tu baada ya kuvua nguo kwa sababu ya tofauti ya joto ni rahisi kupotosha majibu ya kipimo. Usifanye maamuzi kutokana na uume teke.


Kamwe usilinganishe urefu wa uume teke na urefu wa uume uliosimama, kwa sababu wakati fulani uume teke unaweza kuwa mkubwa na mrefu kuliko uume uliosimama na hata kinyume chake.
Ukubwa wa uume unategemea:
Kiwango cha ukubwa wa uume kinategemea na kiwango cha mhemuko, muda wa siku, joto la kawaida, mara ngapi unafanya tendo la ndoa , na uhakika wa kipimo.


Hakuna takwimu za urefu wa uume kwa vijana kwa sababu watu hukua kwa viwango tofauti.


Kwa watu wazima, wastani wa ukubwa wa uume uliosimama ni kati ya 14-16cm (5.5-6.3 inch). Wastani wa upana kwa uume uliosimama ni 12-13cm (4.7-5.1 inch). Wastani wa uume teke unaweza kuwa kati ya 3.5-3.9 inchi. Uume unachukuliwa kuwa mdogo (micropenis) iwapo uko chini ya inchi 3.


Uzoefu katika mapenzi
Badala ya kupima ukubwa wa uume wako, jaribu kutafuta G-spot,kumchezea mpenzi katika maeneo yanayosisimua. Kumchezea mwanamke ni muhimu ili aweze kufikia kileleni. Endelea kuwa nasi kupitia Tazama Line kioo cha jamii.