Sunday 8 February 2015

PICHA ZA NGONO ZA NAY ZAMLIZA MCHUMBA’KE!

Udhalilishaji! Picha za ngono zilizozagaa katika mitandao ya kijamii za Staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’,
zikimuonesha akifanya ufuska na mrembo chumbani zimemliza mchumba’ke, Siwema ambaye ameamua kumsusia mtoto wao mchanga.
Staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, akifanya ufuska na mrembo chumbani.
Habari kutoka chanzo cha kuaminika zilimiminika kwamba, baada ya kusambaa kwa picha hizo kuliibuka tafrani nyumbani kwa wapenzi hao, Kimara jijini Dar ambapo Siwema alidai kuondoka usiku wa manane akimwacha mtoto mchanga.
Baada ya kupata habari hiyo gazeti hili lilimtafuta Nay ili kuzungumzia sakata hilo ambapo alikiri kuzijua picha hizo lakini akashangaa ni nani aliyempenyezea umbeya mchumba’ke na kwamba ni kweli mama mtoto wake huyo alilia japokuwa alitumia nguvu
kubwa kumweka sawa na sasa maisha yanaendelea.
‘Nay wa Mitego’ akiwa na mchumba’ke, Siwema.
Kwa upande wa Siwema alisema: “Nay amenipa maelezo juu ya picha hizo ingawa tulikuwa tumefikia pabaya sana kiasi cha kutaka kuondoka kwake lakini kanielewesha.