Thursday 12 February 2015

MTANGAZAJI MAARUFU WA TELEVISION AJIACHIA SEHEMU NYETI BILA KUVAA KUFULI


Presenta wa Kipindi cha Nyumbani ni Nyumbani katika Kituo cha Runinga cha C2C cha jijini Dar es Salaam, Lulu Mathias Semagongo ‘Aunt Lulu’ (pichani) amewashangaza watu baada ya kukaa vibaya huku akiacha wazi maungo yake nyeti.

Tukio hilo lililoshuhudiwa na Paparazi wetu lilijiri ndani ya ‘kiwanja’ cha starehe cha Billicanas kilichopo Posta, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.

Katika tukio hilo, kachero wetu alimshuhudia Aunt Lulu akiwa hana tone la aibu usoni huku baadhi ya watu wakiponda kivazi alichotinga ambacho mbali na kumwacha uchi kwa asilimia kubwa lakini pia kilimchora akiwa hana hata ‘kufuli’.
“Hiyo , naamini kabisa ni mwisho wa dunia kwa staili hii, wewe angalia msichana kama yule anatembea uchi na mbaya zaidi hana nguo ya ndani,” alisikika mrembo mmoja aliyemwona Aunt Lulu ukumbini humo.

Kama kawa kama dawa, Risasi Mchanganyiko ‘lilimtaiti’ Aunt Lulu na kumhoji kulikoni kukaa uchi ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Siko hapa kwa ajili ya kujibu maswali, niko kistarehe zaidi.”