Tuesday 14 October 2014

HUYU NDIYE KIJANA ALIYESABABISHA MWANADADA HUYU WA CHUO CHA UHASIBU SINGIDA KUJICHOMA KISU KISA KUMTOLEA NJE.

Mwanadada Moza Kassim mwanafunzi wa chuo cha Uhasibu Tawi la Singida, inadaiwa kuwa usiku wa ijumaa kuamkia jumamosi iliyopita mkoani Singida, alijibizana na mpenzi wake ambaye eti aligundua kuwa ana mpenzi mwingine na katika vuta ni kuvute hawakufikia muafaka ndipo mwanadada akamwambia mpenzi wake kuwa anajichoma kisu mwanaume akajua ni utani akamjibu huwezi, mwanadada akamwambia kwa mara ya pili kisha Moza akajipiga kisu tumboni karibu na kiuno hali yake ikawa mbaya na kuanza kuchuruzika damu ikabidi rafiki zao waliokua karibu wakamkimbiza hospitali ya mkoa, na jana alihamishwa hospitalini hapo na mwanadada huyo yupo chini ya ulinzi wa jeshi la polisi, na kwa mujibu wa sheria Moza ana kesi ya kujibu.