Wednesday 22 October 2014

ETI WANAUME NI VIUMBE WABINAFSI SANA WASIOJUA UTU.... ''I REAL HATE YOU MEN''

Najitahidi sana kuamini kuwa wanaume ni wazuri ila kila kukicha naona hawa viumbe ni wanyanyasaji, wabinafsi, hawana utu, wauwaji, wabakaji, wanyaganyi, wauwaji, roho mbaya.


Nitaendelea kuamini wanawake ndiyo chachu ya maendeleo hasa kwa watoto wao.

Mtabishana a mimi lakini ndiyo ukweli wenyewe baba anatelekeza watoto anamwachia mama. Mama kwa kujali na upendo anaamua kupambana na baba atoe matumizi ya familia ada ya shule huku lijianaume likiwa libishi kuendekeza ufuska tu.

Leo hii nyie nyie wanaume mnakuja na viutafiti vyenu eti watoto wliolelewa na mzazi mmoja wanatatizo mfyuuu hata aibu hamna.

Asilimia kubwa ya watoto wengi ni mapambano ya mama kuvumilia uozo wote wa baba na kujitahidi kukufanya kama ulivyo mwisho wa siku mnajifanya kufanya utafifi.

Suluhisho kila mwanaume anayetia mwanamke mimba ahakikishe anakuwa bega kwa bega na mama hata kama unanyimwa papuchi, hata kama hupendi mama, matatizo yako na mama yasipelekee shida kwa watoto.

I real hate you men