KANISA la Presbyterian nchini Marekani ambalo lina wanachama milioni mbili, limebadilisha sheria yake ya ndoa
na kuwajumuisha watu wa jinsia moja.
na kuwajumuisha watu wa jinsia moja.
Kanisa hilo ambalo linashirikisha idadi kubwa ya wanachama wake duniani lilitoa tangazo hilo baada ya idadi kubwa ya magavana wa majimbo yake 171 kuidhinisha mabadiliko hayo.
Sheria yake mpya sasa itasoma kwamba ndoa ni makubaliano ya kipekee kati ya watu wawili ikilinganishwa na makubaliano kati ya mume na mke.
Sheria hiyo iliyoidhinishwa na baraza kuu la kanisa hilo mwaka uliopita ilikubaliwa na zaidi ya nusu ya majimbo ya kanisa hilo.
Uamuzi huo unatarajiwa kuzua mgawanyiko
mkubwa kati ya wanachama wa kanisa hilo ambao wanapinga sheria hiyo.