Saturday 20 December 2014

MASOGANGE NDANI YA KASHFA NZITO NCHINI AFRIKA KUSINI...SOMA MKASA MZIMA HAPA

Video Queen matata Bongo, Agnes Jerald ‘Masogange’.
VIDEO Queen matata Bongo, Agnes Jerald ‘Masogange’ amefungua mdomo wake na kuwaka kuwa anachukizwa na tabia ya baadhi ya watu ambao wanatumia jina lake kutapeli kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Masogange alisema kuwa watu wanaotumia jina lake wakome kwa sababu wanamjengea hisia tofauti kwa watu wakati yeye hanufaiki na chochote. 
“Kwa kweli inauma sana mtu kutumia jina langu kwenye mitandao halafu halitumii kwa uzuri, kazi ni kuomba pesa kwa watu mbalimbali, jamani mimi situmii mtandao wa Facebook kabisa kwa hiyo watu wawe makini,” alisema Masogange