Tuesday 16 December 2014

KAKA BADILIKA, UTAFIKIRI TAA YA TRENI

Haya tena wapenzi tumekutana tena kama ilivyo ada anti yenu nimejaa tele kama pishi ya mchele, nakushangaa wewe, eeh wewe unamuangalia
nani? Kila siku kulalama eti mke wangu kanichoka, mchezo kama mgao wa umeme.
Wan’chekesha tena wan’chekesha sana, jamani tokea lini tembo akaelemewa na mkonga wake au kuku alikufa kwa kutambaliwa na utitiri.
Leo nataka nikupashe upashike hata katika mpira kila kukicha wanabadili muundo wa mchezo uwanjani. Enzi za 4-2-4 zimepitwa na wakati siku hizi utasikia sijui kuna 4-4-2  au 3-5-1  na mwingine sijui unaitwaaa, eeh nimekumbuka 4-3-3.
Sasa wewe mwenzangu umekalia mtindo mmoja wa toka ubalehe, wa kifo cha mende kama taa ya gari moshi ambacho sijawahi kusikia mazishi yake. Jamani kama mfumo wa kuleta raha uwanjani ulibadilika kwa nini na wewe usibadilike.
Siku hizi dunia imeendelea, kila siku mambo yamebadilika na watu wanakwenda na wakati, tulikuwa Analojia sasa mambo yote Dijitali au siyo jamani bila king’amuzi hupati picha. Mwanaume lazima uwe mbunifu kujua mpenzi wako anataka nini au anakosa kitu gani.
Nasikia kuna baadhi ya wanawake wamezidi ubishi wakielezwa geuka hivi eti usumbufu, nani alikuambia mapenzi ni mchezo wa kujipikilisha. Napenda nikueleze na wewe unayejifanya kazi yako kumsubiri mwenzio atue mzigo kisha ateremke.
Dada wee, uguswapo sisimka pandisha mzuka na kujituma muda wote, hakikisha uliye naye anafurahia kuwa nawe, siyo mtu anafanya ili kukamilisha zoezi. Haipendezi, raha ya pilipili utoe mlio wa kuwashwa kila mtu ataijua kweli pilipili kali.
Lazima niseme ukweli mapenzi si lelemama, usione mwanamke kanunuliwa nyumba au gari, hakupata kwa njia ya mkato, kajituma mwakwetu. Ukijua kukitumia kitanda vizuri kinajua kulea ndoa acha kuringia umbile ukadhani ndilo lililobeba ndoa. Siku zote  utamu wa muwasho ukunwe na mwenye kucha fupi.
Sikupenda kulizungumzia hili leo kazi yangu kubwa ilikuwa ni kwa hao kina baba wanaojifanya kazi yao kumwaga mzigo na kuondoka huku kila siku mtindo uleule kifo cha mende na mbuzi kagoma kwenda. Najiuliza siku mende asipokufa au mbuzi akikubali kwenda itakuwaje?
Wote wanajua kumfikisha mtu juu ya mnazi,  lakini utundu ndiyo humfanya mtu ajiulize mara mbili hiki nipewacho wote wanapata kama hivi au raha hizi ni wote wanaoinjoi kama mimi, je, nikimpoteza nitampata kama huyu?
Mwanaume unatakiwa uwe mtundu kwa kulianzisha kwa mpenzio kwa mazingira yoyote, usisubiri kitandani tu na mtindo wako mmoja kama taa ya gari moshi.Nayasema haya siku moja nilikutana na mtu mmoja katika pitapita yangu enzi za ujana ambaye nilimpa majina ya bwana mitindo.
Wee acha, kuna wanaume wameumbwa kwa kazi hiyo utafikiri alisomea tumboni kwa mama yake.
Hukuwepo shetani wako alikuwepo, nilikutana na mitindo zaidi ya 50 na kila mtindo ulimzidi mwenzake na ulikuwa na jina lake. Kwa vile ni zamani nilikumbuka michache.
Kuna Punzu maguru, Kolandoto, General Tyre, Biasenza, Goliko na mingine mingi. Mmh!  Wee acha tu, kwa kweli ukikutana na mwanaume mtundu kama huyo huwezi kutoka nje ya uhusiano wako.
Nalisema hili kuwakumbusha wanaume waache kufanya mapenzi kwa mazoea, alichokikuta basi hichohicho, kuna mwanamke bila kumkunja kama mkizi hajisikii raha nawe umeng’ang’ania kifo cha mende basi hata ungebadili baada ya kifo cha mende uongeze mazishi ya mende kila siku mende anakufa atazikwa lini.
Yangu kwa leo naishia hapa narudia kauli yangu ya kila siku, kuku hafi kwa utitiri na punda hafi kwa kupigwa. Jamani teknolojia imebadilika tangu analojia mpaka dijitali.