Saturday 13 December 2014

ETI YADAIWA ELIZABERTH MICHAEL (LULU) NA MSHINDI WA BBA IDRIS WANAJIUSISHA NA CHAMA CHA FREEMASONS..USHAHIDI HUU HAPA


Cheni (Mkufu) wa LULU wazua utata. Wengi wasema ni kama wa IDRIS. Wachache wadai eti ni FREEMASONS
Baada ya mwanadada LULU kutupia picha yake mpya kwenye mtandao akiwa amevaa cheni ama mkufu  mpya shingoni mwake, maswali kadhaa ya wadau yameanzaje kujitokeza kuhusu cheni hiyo pamoja na maana yake.

Huku kukiwa bado kuna vuguvugu la ushindi wa Tshs.  MILLIONI 500 za kijana Idris toka jumba la BIG BROTHER na lulu akiwa ni mmoja wa watu wakubwa sana waliokuwa wanawahimiza wananchi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania na mipaka yake kumpigia kura kijana huyu ili ashinde, maswali Kadhaa yamejitokeza kuhusiana na mkufu huo ulioko kwenye shingo laini ya mrembo LULU.
1. Swali kuu la kwanza?
Je, LULU kanununua mkufu wenye alama hiyo ili ufanane na ule wa Idris aliyeshinda million 500? kama mpango yakinifu wa kujiweka karibu na ‘Millionea’ huyo?
2. Swali kuu la pili?
Lulu kajiunga FREEMASONS? Mbona mkufu wake huo una alama zao zile zaoo?
Tusaidie ndugu msomaji kwa maoni yako hapo chini…