Saturday 20 December 2014

Idris Awapiga Chini Goitse na Ellah na Kumtambulisha Rasmi Samantha Ukweni!

Mr Lover Man kwa sauti ya IK, Idris Sultan ameamua kuchagua moja (kwa sauti ya Fid Q). 

Baada ya kubadilisha title na kuwa milionea, Idris ameamua kumleta nyumbani mrembo wa Afrika Kusini, Samantha au kwa lugha ya vijana wa kisasa ameamua kumfanya ‘main chick’ na kutuachia kitendawili kama Goitse Kgaswane wa Botswana na Ellah wa Uganda watakuwa ‘side chicks’ ama wamepokea kibuti rasmi.

    Shocked by the size of this pineapple though. I feel like my whole life has been a lie. #tanzanianthings pic.twitter.com/MT9eAOP6PA

    — Samantha BBA HotShot (@SamanthaJay17) December 16, 2014


Samantha alitua Dar Jumatatu hii na mwenyeji wake amekuwa akimzungusha kwenye kwenye maeneo muhimu ya mji huu wenye joto kama jangwa la Kalahari. Na Samantha ameweka wazi rasmi kuwa anaipenda Tanzania.


    Tanzania nakupenda Sana