Hivi karibuni Femcee anayetesa kwenye anga za Rap nchini Marekani Nicki Minaj anayeitendea haki vilivyo label ya YMCMB alitangazwa kuachana na ‘Boyfriend’ wake wa zaidi ya Miaka kumi anayefahamika kwa jina la Safaree Samuels.
Kuachana kwa wawili hawa kumetangazwa sana kwenye mitandao na magazeti pamoja na vyanzo tofauti vya media ulimwengu mzima lakini haijawahi kufahamika wazi nini hasa chanzo cha wandani hawa kuamua kuupiga stop uhusiano wao .
Imefahamika kuwa chanzo cha wapenzi hawa kuachana ni kitendo cha Nicki Minaj kumletea jamaa wake ‘swagger’ za kimtaa kimtaa baada ya kugundua kuwa ana nyendo tofauti na madem wengine .
Stori ni kuwa Nicki kuwa alichukua gongo linalotumika kwenye mchezo wa baseball maarufu kama ‘Baseball Bat’ na kumfukuza Safaree akimkimbiza kutoka nyumbani kwake .
Kana kwamba hiyo haitoshi; Nicki aliingia kwenye sehemu ya kupaki magari ambako alimalizia hasira zake kwenye gari ya kifahari ya jamaa huyo aina ya Mercedez Benz ambapo aliishambulia kwa nguvu zake zote na kuiharibu.
Baada ya hapo wapenzi hawa wameachana na hakuna dalili zozote za kurudiana japo huwezi jua , chochote kinaweza kutokea.