Sunday 2 November 2014

HUU HAPA UKWELI KUHUSU WADA WA KAZI ZA NYUMBANI..(HOUSEGIRLS) WA SIKU HIZI

Zamani miaka hiyo kulikuwa hakuna uhaba wa madada wa kazi na zamani kufeli darasa la saba haikumaanisha hauna akili bali shule za sekondari zilikuwa chache


Tangu mpango wa elimu wa shule za msingi na ule wa sekondari sijui wanaita mesi sijui mmes sijui nini

vijiji vyote hata vile visivyojulikana vina shule za msingi na kila kata kuwa na shule hata mbili za sekondari ni kawaida

Tumeshuhudia sasa hata wasiojua kusoma wanafaulu kwenda sekondari

Mabinti hawa wakimaliza kidato cha nne huwa hawataki kufanya kazi za ndani kwani anaweza kwenda polisi ualimu,unesi au hata kuwa secretary au hata kuuza kwenye stationery etc

Madada wengi wa kazi wa miaka ya karibuni ni wale waliofeli darasa la saba wasiojua hata raisi wa Tanzania ni ...... 

Anayefeli darasa la saba kwa miaka hii ujue ni kilaza namba moja hafai hata kuachiwa nyumba
Ndio maana wadada wa kazi za ndani siku hizi hawapatikani kirahisi na wakipatikana huwa hawaperform kama wazamani kwa sababu ni vilaza walioshindwa hata kujua mlima mrefu kuliko wote afrika.