Friday 22 July 2016

Wanawake wa Stahili Hii, Wanakera Mno

Mwanamke nimemtongoza kanikubalia, nikamuomba mzigo kanibania, alafu muda mwingi anaokutana na mimi anakifanya ana haraka muda mwingi utamsikia akisema 'nataka kuondoka lakini nina haraka' as if mmekutana bahati mbaya.

Basi unapozidi kumbembeleza, we unaongea naye ye yuko busy anachat kwa text na watu wengine na ninapojitahdi kutaka kugundua anachat na nani, ndivyo simu yake anaiweka mbali na upeo wa macho yangu.

Mara nyingi mimi ndo wa kwanza kumshtua kene simu kila siku, nisipofanya hivo siku inapita na ninapomuulza kama ananipenda anajibu ananipenda. Naomba mnisaidie huyu binti ananipenda kweli? Au yupo kimaslah zaidi?

Ushauri kwa mabinti kama mwanaume huwezi kumpenda au haujakidhi vigezo vyako, mtose siku ileile ya kwanza sio kukubal Kinafiki.