Wednesday 16 November 2016

Mange Kimambi Aikosoa Ziara ya January Makamba Studio ya Wasafi Records, Adai Ameenda Kumpoza

Siku kadhaa zilizopita Mh January Makamba alitembelea Studio ya Wasafi inayomilikiwa na Msanii Diamond Platnumz, Watu mbali mbali wametoa maoni yao akiwemo na Mange Kimambi ambaye ameandika haya hapa chini kuhusu ziara hiyo:

Mangekimambi_
"Kwanza nianze Kwa Kusema this is not about Diamond, it's about viongozi wasiojielewa . So watu wa mateam mkileta viranga ni block tu.

Naomba kuuliza Waziri wa mazingira anafanya nini ofisi Za WCB??? kulitokea tetemeko huko WCB? Au vyoo vyao vimeziba kutokana na mazingira? Au??? Mara 100 ingekuwa Nape, tungemchamba nae Ila angalau yeye ni department yake, Makamba anahusika vipi na studio za wanamuziki wa Tanzania??? Kama anaweza kuacha kazi Za wizara yake akaenda kuuza sura mtaani why asiende sehemu ambazo wanyonge wanateseka? Why asiende Muhimbili akawaone wale ndugu Za Wagonjwa wa mikoani wanaolala barabarani nje ya hospitali?? why asiende ocean road akaone watanzania wanavyokufa Kwa kukosa huduma sababu hospitali ni ndogo Na wagonjwa ni wengi, Kila Mwaka watanzania 20,000 wanaachwa wafe Na cancer bila kupata mionzi sababu hospitali haiwezi kuhudumia watanzania Wote, why asiende huko? Hii Ndo serikali ya kutetea wanyonge?

Ngojeni niwaambie kilichompeleka January Makamba ofisi za WCB. Kaenda kichama Kama CCM , Yani Huyu kiongozi hayuko Kwa ajili ya kusaidia watanzania yuko Kwa ajili ya Chama tu. Same way Na Nape Kila nachofanya ni Kwa Akili ya Chama sio watanzania, Kilichompeleka January WCB ni Diamond kuichana serikali kwenye radio last week. Diamond alikaliwa shingoni na TRA alipe kodi ya milioni 236.Akawa anasema hana, Diamond akaenda kwa Kikwete, Ndo ile Safari na vijana wake walivyoenda nyumbani kwa JK, walikuwa wameenda kumuomba Kikwete awaombee kwa Magu wasilipe hiyo kodi au ipunguzwe, Kikwete akasema Hapana hawezi kuwaombea. Ndo Dai ikabidi achukue mkopo kiasi akachanganya na pesa zake ndo akalipa Hiyo kodi.Baada ya kulipa Hiyo kodi ndo Dai mapovu yakawa yanamtoka balaaaa kuhusu serikali na makodi, Ndo mpaka last week akawachana mbayaaa kwenye radio. Unaambiwa Dai kaongea kishenzi akawa anasema hawasupport tena CCM Ndo mnamuona January huyo mbiooo kaenda kuua sooooo maana wasije kumpoteza Diamond kwenye Kampeni ya 2020.Dai Alisema kabisa redioni anatamani mpaka ahame Chama, ndo CCM wanamlambalamba asiende upande wa pili, nahisi next time itabidi wamsamehe kodi maana kajua kuwatetemesha, mpaka Waziri wa mazingira kaenda studio za mziki" Amedika Mange Kimambi katika ukurasa wake wa Instagra