Wednesday 1 April 2015

Dillish: Hela Nilizoshinda Big Brother Afrika Zimekwisha Zote


Dillish Mathews, mshindi wa shindano la Big Brother Africa mwaka juzi, amedai kuwa amemaliza fedha zote alizoshinda.

Mrembo huyo wa Namibia aliyejishindia zaidi ya shilingi milioni 500 amepost video kwenye mtandao wa Instagram na kuongea maneno ambayo wengi wamechukulia kama utani kuwa hana tena fedha hizo.

“About what I did with my money that I got from Big Brother? It’s finished. A couple of Rolexes, kept going to Milan, London, Hong Kong, Shanghai…it’s finished. Kapu,” anasikika akisema kwenye video hiyo.

Kwenye video hiyo aliandika: Read on social media im broke… So here it is just in case your life depended on it. I don chop finish”

Hata hivyo wengi wamekerwa na kauli yake.