Naombeni ushauri wenu,
Mawazo ya wengi ndio nitakayoyafanyia
kazi. Nimefunga ndoa na mwanaume
mwenye watoto 4 wawili wakike wawali
wa kiume. Mama yao alifariki kwa ajali ya
gari aliwaacha wadogo wakiwa primary.
Na mimi niliolewa nikiwa na mtoto
mmoja wa kike ambae kiumri
analongana na mtoto wake watatu.
ngumu sana kukubali ombi lake hasa
nikifikiria kulea watoto wa mama
mwingine wanikubali, je, vipi kuhusu
huyu nilienae?
Baada ya muda kupita na kukolea
kimapenzi nilijubaliana nae tukafunga
ndoa tukaunganisha familia wote
wakawa kitu kimoja. Mungu akabariki
tujaliwa kupata mtoto mmoja. Kiukweli
niliwapenda sana hawa watoto,
niliwalea kama wangu.
Nilijitahidi kadri ya uwezo wangu
kuwafanya wasijione wakiwa. Kama
zawadi nk nilitowa mezani bila kubagua
sikupenda kuweka makundi na hili
shahidi ni Mungu pekee. Watoto watatu
wapo chuo kikuu na mmoja wa kwake
yupo form six.
Katika ndoa yangu kulikua na
migongano upande wa tendo la ndoa,
kabla ya ndoa tukiwa kwenye stori za
mapenzi niliwahi kumweleza
mwenzangu kuwa mimi sio mtundu
sana upande wa sex ivyo ningependa
yeye awe mwalimu kwangu kwani
tangu mwanaume wa kwanza
anidanganye na kunipa ujauzito sikuwa
tena kuwa na byfriend.
Akiniambia sawa. Tulipoingia kwenye
ndoa mwenzangu alianza kubadilika
wakati mwingine alikaa hata miez 8-10
bila kutaka sex.Nikimuuliza husema
amechoka au hajisikii.
Hata huo muda anaokaa mpaka mimi
nimchokoze na hii nikutakana na
kushindwa kuvumilia. Kuna wakat
aliamua kuniambia ukweli kuwa sijui
mapenzi, niliumia ila nilikubali kuwa ni
kweli sijui ila anisaidie kujua.
Hakufanya ivo. Ilifikiwa wakati nikaona
ngoja nikae nisimsumbue ila nilijiuliza
nitaishi hivi mpaka lini na kusaliti ndoa
siwezi. Nilimwomba Mungu sana anipe
uvumilivu ila pia Mungu aseme na mimi
juu ya hii ndoa.
Mungu ni mwaminifu. Baada baada ya
maombi ya zaidi ya mwaka mke wa
shemeji yangu alileta malalamiko kuwa
mume wangu amekua akimsubua sana
kimapenzi ikiwa ni pamoja nakumtumia
picha za ex.
Niliziona hakuishia hapo akasema hata
hawa wadada wa kazi huwa anatembea
nao. Nilipowabana waliopo na
walioondoka walikubali na kunipa
ushahidi. Mbaya zaidi hata huyu
mwanangu alishamtaka kimapenzi sina
uhakika kama alifanikiwa au la.
Ninaumia sana sana. Mtaani ndoa yangu
imekua mfano wa kuigwa hio ni
kutokana na jinsi tunavoonekana kwa
watu. Lakini hii yote onatokana na jinsi
nisivopenda watu wajue mambo ya
ndani. Ninampenda, ninamheshim,
ninamjali.Siruhusu nguo au chakula cha
mume wangu afanye mwingine
nikiwepo.
Hata kama tumegombana nisingependa
yoyote ajue, nilijitahidi sana, kuwa mtiifu
na mnyenyekevu kwake. Hii nikutokana
na malezi niliyolelewa. Hata kama
amesafiri watoto watajua baba anarudi
kwakua wataniona jinsi ninavokua busy
jikoni na kuandaa juisi na matunda.
Ushauri wenu muhimu sana kwangu
Asanteni